Tue, 19 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga Yusuph Athuman na Erick Mwijage ali-yekuwa anakipiga Kagera Sugar wame-pewa mkono wa kwa heri katika timu waliokuwa wakitumikia ya West Armenia FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Armenia huko Ulaya Mashariki.
Wakati wanajiunga na timu hiyo Julai mwaka huu wote walipewa mkataba wa miaka miwili.
Wachezaji hao Wakitanzania wamepewa mkono wa kwaheri mara tu baada ya Ligi Kuu ya Armenia kumalizika huku timu hiyo ikimaliza nafasi ya 8 kati ya timu 10, ikivuna pointi 17 katika mechi 20, ikishinda 5, Sare 2 na kupoteza mechi 13.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live