Mon, 26 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu nchemba leo Jumatatu Juni 26, 2023 amesema katika mwaka wa fedha unaoisha maendeleo yametokea katika sehemu nyingi ikiwemo sekta ya michezo kwa Yanga kufanya vizuri kitaifa na kimataifa.
“Maendeleo yametokea katika sekta nyingi na Watanzania wote mashahidi, hata Yanga kufika fainali na kuchukua vikombe vyote ni hatua ya maendeleo ambayo haijawahi kufikiwa,”amesema.
Mwigulu amesema hayo akijibu hoja mbalimbali zilizoibuliwa na wabunge katika majadiliano ya bajeti hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live