Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwigulu:Natamani nembo ya Yanga iwepo kwenye noti

Mwigulu Yangaaaaaaaaaaa Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba

Thu, 13 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

“Mafanikio ya Yanga na Klabu nyingine yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na hamasa ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia ambapo amekuwa akitoa shilingi milioni tano kwa kila goli linalofungwa katika hatua ya makundi na shilingi milioni kumi kuanzia hatua ya robo fainali. Hivyo, kwa namna ya pekee naomba nitoe pongezi kwa Mama yetu kwa ubunifu huo ambao umeliletea Taifa letu sifa na heshima 164 kubwa katika nyanja ya michezo”

“Rai yangu kuwa tuendelee kuhamasisha michezo mingine ili Nchi yetu iweze kushiriki katika mashindano mbalimbali ya kimataifa na hatimaye kurudi na tuzo au makombe, aidha napenda kutumia fursa hii kuipongeza Timu ya YANGA kwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya kandanda nchini kwa mara ya tatu mfululizo na Kombe la Shirikisho la Benki ya CRDB”

“Yanga ni Wafalme wa soka la Tanzania, natamani kumshauri Gavana wa Benki kuu kuweka nembo ya klabu ya Yanga kwenye noti ya shilingi 100 kuyaenzi mafanikio haya” Dr. Mwigulu Nchemba.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: