Naibu Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amelitaka Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Kuhakikishe kuwa wanakutana na Chama cha Mbio za Magari nchini (AAT) ili kuangalia namna ya kukisaidia Chama hicho kipate hekari 20 zilizoombwa kwa ajili ya eneo la mashindano na mafunzo.
Naibu Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amelitaka Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Kuhakikishe kuwa wanakutana na Chama cha Mbio za Magari nchini (AAT) ili kuangalia namna ya kukisaidia Chama hicho kipate hekari 20 zilizoombwa kwa ajili ya eneo la mashindano na mafunzo. Amesema Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imepewa jukumu la kusimamia michezo yote nchini ili iwe na ufanisi mkubwa kwa kuwa michezo ni ajira kutokana na mchango wake katika mapato ya nchi.