Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwamuzi aliempiga kiwiko Robertson apeta

Andy Robbo.jpeg Mwamuzi aliempiga kiwiko Robertson apeta

Sat, 15 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shirikisho la Soka (FA) limethibitisha kuwa Constantine Hatzidakis hatakabiliwa na adhabu yoyote kwa kuonekana akimpiga kiwiko beki wa Liverpool Andrew Robertson.

Tukio hilo lilitokea wakati wa mapumziko wakati Liverpool ilipotoka sare ya 2-2 na vinara wa Ligi kuu ya Uingereza siku ya Jumapili, huku Robertson akimsogelea Hatzidakis, mwamuzi msaidizi, ambaye baadaye alionekana kuinua mkono wake juu kwa kiwiko chenye ncha kuelekea kwa nahodha wa Scotland.

FA ilianzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo na kusema Hatzidakis hatapewa mchezo wowote hadi utakapokamilika.

Siku ya jana, ilithibitishwa kwamba afisa huyo hatachukuliwa hatua zaidi, na taarifa ikisomeka:

“Tumepitia kwa kina ushahidi wote kuhusiana na tukio la hivi majuzi huko Anfield linalomhusisha beki wa Liverpool Andrew Robertson na afisa wa mechi Constantine Hatzidakis, na hatutachukua hatua zaidi.”

Mchakato wetu wa kina ulihusisha kukagua taarifa za kina kutoka kwa Liverpool na PGMOL, pamoja na pembe nyingi za picha za video, kuhusiana na tukio na mazingira yake.

Hatzidakis pia alitoa taarifa kupitia PGMOL, akieleza kwamba alikuwa ameomba msamaha kwa Robertson alitaka kuchora mstari chini ya tukio hilo akisema kuwa hakika haikuwa nia yake kufanya mawasiliano yoyote na Andy alipouvuta mkono wake kutoka kwake na kwa hilo ameomba msamaha.

“Nilisaidia FA kikamilifu katika uchunguzi wao na tumejadili suala hilo moja kwa moja na Andy Robertson wakati wa mazungumzo ya wazi na mazuri. Hakika haikuwa nia yangu kufanya mawasiliano yoyote na Andy huku nikiuvuta mkono wangu kwake na kwa hilo nimemuomba msamaha.”

Natarajia kurejea kwenye mechi za wasimamizi. Alimaliza hivyo mwamuzi huyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live