Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwamnyeto: Siondoki Yanga mpaka wanifukuze

Mwamnyeto 10 Milioni Mwamnyeto: Siondoki Yanga mpaka wanifukuze

Wed, 15 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Beki wa kati na nahodha wa Klabu ya Yanga, Bakari Nondo Mwamnyeto amekana tetesi zinazosambaa kuwa huenda msimu ujao akaibukia kwa wapinzani wao Simba SC.

Mwamnyeto amesema hayo baada ya Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa mara ya 30 baada ya kuitungua Mtibwa Sugar mabao 3-1 katika Dimba na Manungu, Turiani mkoani Morogoro.

“Kucheza kwenye kikosi ambacho kina ushindani mkubwa wa namba sikuwa na presha yoyote, nimeshacheza mechi nyingi sana na wachezaji mbalimbali, kikubwa ni umhimu wa mechi kulingana na mwalimu anavyokupanga, akiona mechi hii unafaa kucheza unacheza, Yanga acheze yoyote sisi shida yetu ni alama tatu basi.

“Kuhusu msimu ujao ninawaambia mashabiki kwamba Yanga Bingwa, sina kingine zaidi. Yanayozungumzwa hayanihusu, Yanga Bingwa… Yanga Bingwa… Yanga Bingwa…. Yanga Bingwa. Siondoki Yanga mpaka wanifukuze wenyewe,” amesema Mwamnyeto.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live