Sun, 9 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwamnyeto Foundation inayosimamia na nahodha wa Yanga Bakari Mwamnyeto pamoja na kiungo wa timu hiyo Zawadi Mauya imetoa msaada katika vituo viwili vya watoto yatima ambavyo ni Mihayo na Mgolole vilivyopo mkoani Morogoro .
Juzi timu ya Mwamnyeto Foundation ilicheza na Timu ya Moro Combine katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro na kufungwa kwa mikwaju ya penati 6-5 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika dakika 90 za mchezo.
Fedha zilizopatikana katika mchezo huo ndizo zimetumika kununulia mahitaji ya kusaidia katika vituo hivyo viwili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live