Golikipa wa Simba SC, Ally Salim amesema kilichomfanya aweze kuchomoa mikwaju ya penalti ya Singida FG ni maelekezo ya mwalimu wake.
Ally alisema Singida walifahamu kuwa anawajua jinsi wanavyopiga lakini yeye alizingatia vile alivyoelekezwa na mwalimu.
"Alinipa maelekezo kwamba fanya hivi fanya hivi, wakipiga fanya hivi na hivi na kweli nikafanikiwa," alisema Ally.
Kwenye mikwaju hiyo mitano iliyoelekezwa langoni kwake, Ally alifanikiwa kuchomoa mitatu kitendo ambacho kiliwafanya wapate ushindi katika mchezo huo wa nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya wachezaji wa Simba kufanikiwa kushinda penalti 3 kati ya nne walizopiga.