Thu, 19 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi maarufu wa soka, Mwalimu Alex Kashasha amefariki dunia leo Agosti 19, 2021 akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Kairuki mkoani Dar es Salaam.
Kashasha alikuwa mtumishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) hadi umauti ulipomfika.
Bado haijawekwa wazi hasa chanzo cha kifo chake, Lakini katika taarifa iliyowekwa kwenye Mitandao ya Kijamii ya TBC, imesema taarifa zaidi zitatolewa.
Marehemu Alex Kashasha amezaliwa mwaka 1957.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live