Wed, 6 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji wa Kimataifa wa Malawi Tabitha Chawinga amechaguliwa kuwa Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Wanawake wa msimu wa 2022-23 nchini Italia kwenye tamasha la usiku la soka nchini Italia.
Tabitha ambaye Msimu huu amesajiliwa na PSG,Msimu uliopita alifunga magoli 23 kwenye mechi 21 alizocheza kwenye Ligi ya Wanawake Nchini Italia na kuibuka kuwa Mfungaji bora wa Ligi hiyo akiweka Rekodi ya Mwanasoka wa kwanza wa Kike kuweza kutwaa tuzo hiyo Italia.
KWA AIBU, Chawinga hayumo kwenye orodha ya wachezaji wanaowania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike wa Afrika wa Mwaka 2023.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live