Sun, 26 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji nyota wa Yanga SC, Kennedy Musonda ameeleza furaha yake baada ya kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC, na kusema kwamba kila mchezo kwenye ligi ya NBC ulikuwa mgumu.
"Kwenye makaratasi unaweza ukauona mchezo utakuwa mwepesi lakini ukawa mgumu au kwenye karatasi ukauona mchezo mgumu lakini ukawa mwepesi," amesema.
Musonda amegusia kwamba kila mchezo timu ilienda na mbinu tofauti kutegemea aina ya mpinzani ili kupata matokeo.
Kwa mtazamo wako, ni mchezo gani ilikuwa mgumu zaidi kwa Yanga msimu wa 2023/2024?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live