Kiungo kipenzi wa Mashabiki wa Yanga, Mukoko Tonombe atakosekana kesho Jumapili katika Kilele cha Wiki ya Mwananchi.
Sababu kubwa ya Mchezaji huyo kukosekana katika tukio hilo la kihistoria kwa Yanga ni kutokana na Mchezaji huyo kuitwa katika maandalizi ya timu ya Taifa.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela amesema kuwa nyota huyo atakosekana kwa sababu ya majukumu ya timu ya Taifa.
"Mukoko anaondoka kuelekea Congo kwenye majukumu ya timu ya Taifa hivyo ni mchezaji pekee atakayekosekana kesho," amesema.
Katika hatua nyingine Mwakalebela amewataka mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi ili kutoa sapoti katika kikosi hicho kinachotarajiwa kucheza na Zanaco ya Zambia.
"Nawasihi mashabiki wa Mwanza, Mbeya, Iringa, Dodoma na kwingineko kujitokeza kwa wingi ili kujionea tamasha kubwa la kihistoria, "amesema.