Tue, 11 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota aliyewahi kukipiga Yanga SC, Mukoko Tonombe, amesema moja kati ya wachezaji waliokuwa wakimpa wakati mgumu akikutana nao ni Mzamiru Yassin na Clatous Chama.
Mukoko ameyasema hayo alipokuwa akifanyiwa mahojiano na Wasafi FM leo Juni 11, 2024 kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo soka.
"Yule mchezaji ambaye huwa pia anacheza timu ya Taifa yule Mzamilu Yasini na Chama wale ni wasumbufu kweli ukikutana nao," alisema Mukoko.
Mukoko aliondoka Yanga na kwenda kukipiga TP Mazembe na sasa amesema yupo huru kwa timu yoyote itakayomuhitaji.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live