Mon, 5 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Yanga, Mudathir Yahya ambaye walimkosa katika mchezo uliopita dhidi ya Kagera Sugar, amerejea kikosini.
Mudathir anatarajiwa kuwepo leo Jumatatu katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Dodoma Jiji utakaochezwa saa 1:00 usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Kiungo huyo alikosekana katika mchezo uliopita kutokana na matatizo aliyoyapata hali iliyomlazimu ashindwe kusafiri na timu kwenda mkoani Kagera.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live