Kiungo wa Yanga, Mudathir yahya Abbas amesema kuwa alitamani kucheza na feisal Salum Abdallah 'Fei Toto' kwenye klabu moja lakini bahati mbaya walipishana wakati wa usajili.
Mudtahir ambaye aliwahi kusema kuwa anatamani kucheza na Fei kwa sababu hajawahi kucheza naye licha ya kwamba wote wanatoka Visiwani Zanzibar.
“Ingekuwa vizuri zaidi kwa sasa tungekutana kwa sababu sote ni wa nyumbani. Kiufupi Ligi inamalizika, tunakwenda kukutana Zanzibar Heros, mtaona ushirikiano wetu,” amesema Mudathir.
Itakumbukwa kuwa, wakati Mudathir anatoka Azam FC anakwenda Yanga, Fei Toto yeye aliondoka Yanga na kwenda Azam FC.