Tue, 24 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Yanga SC, Mudathir Yahya amesema kuwa licha ya kuonekana anacheza vizuri toka ajiunge timu hiyo lakini bado hajawa fiti kama walivyo wachezaji wenzake kutokana na kuwa alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu.
"Nashukuru kwa kupokelewa vizuri Yanga naimani kila mechi zinavyozidi kuja nitaendelea kujitoa kadri atakavyonijalia Mungu.
"Ni kweli sijawa fiti kama walivyokuwa wenzangu lakini muda unavyozidi kwenda nitabadilika," amesema Mudathir wakati akihojiwa Yanga TV.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live