Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Muda wowote Simba Sc watamtambulisha

Ayoub Lakred 1138 Chrome Muda wowote Simba Sc watamtambulisha

Sat, 12 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Simba wanatarajia muda wowote kumtangaza kipa raia wa Morocco, Ayoub Lakred, aliyehudumu takribani misimu minne katika klabu ya mabingwa wa Morocco msimu uliomalizika FAR Rabat. 

Msimu uliopita ndiye aliyekuwa kipa namba moja wa FAR Rabat, akikaa langoni mara 31 ambapo mechi 25 kwenye ligi na 6 kombe la shirikisho wakiishia robo faibali. 

Tangu ajiunge na FAR Rabat kutoka Berkane, amekuwa kipa kinara wa timu, amecheza mechi nyingi zaidi, katika nafasi hii amecheza mechi 100.

kocha wa zamani wa Simba Sven Vandebroeck, anahusishwa na ushawishi wa nyota huyu kujiunga na Simba.Kocha huyo alimfundisha kipa huyo wakati akiwa anaionoa timu FAR RABAT.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live