Sat, 3 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mtoto wa kike wa Nahodha wa Ghana Andre Ayew, Maha Ayew (7) alipoteza fahamu baada ya baba yake kukosa mkwaju wa penati dhidi ya Uruguay.
Binti huyo aliwahishwa hospitali na anaendelea vizuri, na kwa mujibu wa mtoto wa pili wa Ayew. amesema kwamba Maya alianguka mara tu baba yake alipokosa mkwaju wa penati.
Ghana ilishindwa kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya Michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Qatar baada ya jana kukubali kichapo cha magoli 2-0 kutoka kwa Uruguay ambayo licha ya kushinda pia imetupwa nje ya michuano hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live