Sat, 16 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mtibwa Sugar baada ya kucheza mechi 12 imekusanya pointi 5 nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi haijawa kwenye mwendo bora.
Mchezo wake uliopita ubao wa Uwanja wa Majaliwa ulisoma Namungo 1-0 Mtibwa Sugar ambapo aliyekuwa kwenye benchi la ufundi kwa Namungo alikuwa kocha Dennis Kitambi.
Kitambi Desemba 13 alikutana na thank you ambapo timu hiyo Kwa sasa ipo kwenye maandalizi ya mchezo wa Azam Sports Federation Cup dhidi ya Hollywood FC, Desemba 16.
Mtibwa Sugar kituo kinachofuata ni leo Desemba 16 mchezo wa ligi dhidi ya Yanga, Uwanja wa Azam Complex.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live