Sun, 12 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji, Mtibwa Sugar wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Manungu Complex, Turiani mkoani Morogoro.
Mabao ya Mtibwa Sugar leo yamefungwa na Vitalis Mayanga dakika ya 30 na Charles Ilanfya dakika ya 61, wakati la Dodoma Jiji FC limefungwa na Seif Abdallah Karihe dakika ya 90 na ushei.
Kwa matokeo hayo, Mtibwa Sugar inafikisha pointi 29 na kusogea nafasi ya saba, wakati Dodoma Jiji FC inabaki na pointi zake 24 nafasi ya 11 baada ya wote kucheza mechi 23.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live