Mon, 6 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya kuibuka kwa sakata la kalabu ya Machester City kukiuka sheria ya matumizi ya fedha, tayari kuna kila dalili inayoonesha kuwa sakata hilo litaisha kwa maumivu makubwa kwa upande wa kalabu hiyo.
Kwa Mujibu wa Sheria za Premier League, Manchester City hawataruhusiwa kukata rufaa maamuzi yoyote yatakayochukuliwa dhidi yao kama adhabu ya kukiuka kanuni za ushindani wa kibiashara.
Man City wamekutwa na hatia ya zaidi ya makosa mia moja huku wakituhumiwa kwa kutotoa ushirikiano katika kipindi chote cha uchunguzi ambao umechukua miaka minne.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live