Thu, 20 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Al Merreikh imemtangaza Murshid Ally Kika raia wa Tanzania kuwa kocha wao wa viungo.
Murshid ana leseni B ya CAF lakini pia ni mtaalamu wa GPS system za kupima wachezaji
Kabla ya kutua Al Merreikh, aliwahi kuwa kocha wa timu ya vijana ya Zanzibar na klabu ya Kundemba ya Zanzibar lakini akiwa mchezaji alipita timu ya Taifa ya Tanzania U17, Azam Fc na DTB.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live