Thu, 18 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya kupoteza kwenye mchezo wa kwanza. Matumaini ya wachezaji bado ni makubwa kwenye michezo miwili iliyosalia;
Vs Zambia, Vs Congo.
Simon Msuva amesema, licha ya kupoteza, mwalimu ameona mapungufu na watafanyia kazi.
"Bado sisi tuna timu nzuri, tunamshukuru Mungu tumemaliza salama dhidi ya Morocco japo tumepoteza lakini tuna imani tunakwenda kufanya vizuri katika michezo miwili iliyosalia," alisema Msuva baada ya mechi kuisha kwa kupoteza 3-0 dhidi ya Morocco hapo jana.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live