Thu, 4 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Primia Ligi) imekamilisha mechi za raundi ya tano siku ya Novemba 3 kwa michezo mitatu ya Ligi hiyo.
Mpaka sasa kila timu ndani ya Ligi hiyo imecheza michezo mitano. Huku Yanga akiwa ndio kinara ndani ya Ligi hiyo, wakiwa na alama 15.
Tanzania Prisons wanaburuza mkia wakiwa na alama mbili pekee baada ya kushuka dimbani mara tano.
Ligi hiyo kwa sasa itasimama kupisha michezo ya timu za Taifa kufuzu kwa Kombe la dunia Qatar 2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live