Wed, 29 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msafara wa kwanza wa Simba ulioondoka jana jioni Dar es Salaam kwenda Morocco kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Afrika dhdi ya wenyeji Raja Casablanca Aprili 1 umelazimika kuishia Arusha.
Afisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally amesema hiyo imetokana na ndege waliyokuwa wanasafiria kupata hitilafu baada ya kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana jioni.
Matokeo yake utaanza safari leo Machi 29.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live