Wed, 23 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwandishi Fabrizio Romano, Chelsea ipo kwenye hatua nzuri ya kukamilisha uhamisho wa kipa kutoka ligi kuu nchini Marekani kwenye klabu ya New England Revolution, Djordje Petrovic ambaye ni raia wa Serbia mwenye miaka 23.
Taarifa zinasema kipa huyo atasaini mkataba wa miaka saba na kipengele cha mwaka mmoja zaidi.
Chelsea imemtoa kwa Mkopo mlinda mlango wake raia wa Hispania Kepa Arrizabalaga kwenda Real Madrid.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live