Tue, 6 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Television ya SATV imeripoti malalamiko kuwa Rais wa shirikisho la soka Barani Afrika, Patrice Motsepe amekuwa akihudhuria michezo ya timu ya Taifa ya Afrika Kusini mara nyingi kwenye fainali hizi za AFCON.
SATV wanasema hili linawaongezea presha waamuzi na kujikuta wanaipa upendeleo timu hiyo kutokana na uwepo wa Rais kwenye kila mchezo wa timu hiyo.
SATV ipo nchini Morocco na ndio iliripoti tuhuma za kocha mkuu wa kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania Adel Amrouche kuhusu Morocco kuhusika kwenye upangaji wa waamuzi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live