Thu, 3 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya taifa ya Morocco ya Wanawake imefanikiwa kutinga hatua ya 16 kwenye Mashindano ya Kombe la Dunia la Wanawake mara baada ya kushinda goli moja kwa bila dhidi ya Colombia mchezo uliopigwa katika dimba la Perth Rectangular.
Timu tatu pekee kutoka Bara la Afrika zimefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora kwenye Kombe la Dunia la Wanawake 2023.
Hii ni kwa mara ya kwanza timu tatu za bara la Afrika kutinga hatua ya 16 bora kwenye Mashindano ya Kombe la Dunia la Wanawake.
✅ Nigeria
✅ Afrika Kusini
✅ Morocco
Bara la Afrika linaendelea kuonyesha Dunia ubora walionao kwenye soka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live