Morocco wamepanga kutenga bajeti ya kujenga viwanja 2 vikubwa vya mpira wa miguu (Football Stadium).
Viwanja hivyo ili viwe vikubwa kuliko viwanja vyote duniani, Viwanja hivyo Vitakuwa na uwezo wa kupokea mashabiki laki moja na kumi na tatu elfu(113,000) kila kimoja na itawagharimu kiasi cha €500m.
Ujenzi utaanza 2025 na kukamilika baada ya miaka mitatu yaani 2028.
Kumbuka Morocco taifa ambalo limefika hatua kubwa katika historia ya mpira wa miguu Afrika katika final za kombe la dunia(Nusu fainal) watakuwa waandaaji wa fainal za kombe la dunia za mwaka 2030 wakishirikiana na Spain na Portugal