Kocha Mkuu wa Timu ya taifa ya Morocco, Walid Regragui amesema anachofahamu ni kuwa timu yake inapambana kuliwakilisha Bara la Afrika na sio Ukanda wa waarabu kama inavyosemwa na baadhi ya watu.
Baada ya jana kufanikiwa kuiondosha Timu ya Hipsania hapo jana kwa mikaju ya penati kunawalioanza kukejeli kuwa Morocco ni waarabu na hawajivunii kuwa wawakilishi wa Afrika.
"Sipo hapa kujadiri mambo ya siasa, nipo hapa kuhakikisha bendera ya Afrika inawakilishwa vyema kama ambavyo Senegal, Ghana, Cameroon wangefanya" amesema kochu huyo
Morocco itacheza hatua ya Robo Fainali dhidi ya Ureno ya Cristiano Ronaldo Desemba 10.