Thu, 11 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Miamba ya soka la Morocco, Klabu ya Wydad Casablanca wamempatia mkataba wa miaka miwili aliyekuwa kocha wa Mamelodi, Rulani Mokwena ambaye anatarajiwa kuwasili Casablanca leo.
Mokwena alikuwa Kocha Mkuu wa Mamelodi ya Afrika Kusini kwa misimu miwili kabla ya kutupiwa virago mwishoni mwa msimu uliopita.
Msimu uliopita Mamelodi walibeba Ubigwa wa AFL kwa kuwafunga Wydad AC kwa jumla ya mabao 3-2 wakiwa chini ya kocha Rulani Mokwena.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live