Sat, 2 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kapteni Msaidizi wa Simba SC, Mohamed Hussein 'Tshabalala' ameahidi kuondoka na alama zote tatu leo katika mchezo wao dhidi ya Jwaneng Galaxy nchini Botswana.
Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo unaotarajiwa kupigwa leo Desemba 2, 2023 majira ya saa 10 jioni, Tshabalala amesema, wachezaji wote wana morali ya mchezo huo hivyo wanaamini watapata matokeo.
"Uzuri hali ya hewa ni kama ya nyumbani, wachezaji wote morali ipo juu ukizingatia mara ya mwisho tulipokuja kwenye uwanja huu tulipata matokeo, tunaomba mashabiki watuombee inshallah tutashinda," alisema Tshabalala.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live