Mon, 23 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah amepigiwa kura na mashabiki kuwa Mchezaji Bora wa mwezi wa Septemba wa Ligi Kuu ya EPL kwa Wachezaji Soka wa Kulipwa (PFA).
Salah ambaye ni raia wa Misri, amewashinda Haaland, Maddison, Son, Saka na Trippier kushinda tuzo hii.
Salah mwenye umri wa miaka 31 ameichezea Liverpool mechi 11 hadi sasa msimu huu, na amechangia mabao 8 na asisti 4.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live