Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu ya Simba, Mohammed Dewji "Mo Dewji" amelaani kitendo cha Mtendaji mkuu wa Simba Sports Club, mwanamama Babra Gonzales kuzuiliwa kuingia uwanjani Jumamosi ya Disemba 11 kutazama mchezo baina ya Simba na Yanga.
CEO wa Simba Babra Gonzales siku ya Jana ameilalamikia bodi ya Ligi kwa kumkatalia kuingia uwanjani licha ya kuonesha tiketi lakini baadae Shirikisho la Mpira wa Miguu TFF kupitia Afisa Habari wake, walieleza sababu ya Kiongozi huyo kuzuiwa kuingia Uwanjani hapo.
Tazama hapa chini alichokisema Mo Dewji;
Nimesikitishwa sana na kitendo alichofanyiwa CEO wa Simba cha kuzuiliwa kuingia kwenye eneo la VVIP katika mchezo wa jana.
— Mohammed Dewji MO (@moodewji) December 12, 2021
Kwa nafasi ya uongozi aliyonayo Ceo ni jambo la aibu kwa soka letu kukutana na kadhia kama ile. Kumvunjia heshma CEO, nikuvunjia heshma taasisi ya Simba.