Wed, 22 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha ametangaza rasmi kuanza kuiunga mkono timu ya Tabora United kwa kuipatia zaidi ya shilingi milion kumi kila inaposhinda mechi katika michezo mitatu iliyosalia kwenye ya ligi kuu ya NBC,
Chacha ametoa hamasa hiyo mapema leo alipoitembelea timu hiyo ambayo imepiga kambi ikijiandaa kuwakabili Ihefu SC mchezo unaotarajiwa kupigwa kesho Mei 22 kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora,
Tabora United ambao wako nafasi ya 14 wakiwa na alama 26, wanakabiliwa pia na mechi dhidi ya Yanga pamoja na Namungo FC zote ugenini.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live