Wed, 12 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakati taarifa za uhakika zikieleza kuwa Kiungo alieachwa na Klabu ya Simba SC, Jonas Mkude amesaini Klabu ya Yanga.
Sasa taarifa kutoka kwa wasimamizi wa Jonas Mkude kiungo huyo amegomea kukabidhiwa jezi namba 6 iliyoachwa na fundi ‘Fei Toto’
Taarifa zinaeleza Yanga ina nafasi ndogo kumpata staa wa Asec, Mohamed Zoungrana ambaye ndiye waliyempanga kumpa jezi namba 6.
Inaelezwa Mkude amegomea jezi hiyo akidai hataki kuanza na presha ndani ya klabu hiyo kwa kile alichoeleza tayari kuna mashabiki wengi wanasubiri kujua mchezaji gani mkubwa atakabidhiwa namba hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: