Kiungo wa Timu ya Taifa Jonas Gerald Mkude ameomba kuondolewa katika kikosi cha Timu ya taifa ya Tanzania "Taifa Stars" ambacho kimeitwa ili kuingia kambini siku chache zilizopita na Kocha Kim Poulsen.
Taifa Stars inajiandaa na mchezo dhidi ya Benin Oktaba 7, kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia Qatar 2022.
Akizungumzia Sakata hilo, Meneja wa Stars Nadir Haroub Cannavaro amesema Kiungo huyo alifika mpaka kambini na amezungumza na Mwalimu na kumueleza shida yake na mwalimu amemruhusu hivyo ni rasmi itamkosa mchezaji huyo.
Sababu zinazotajwa kumuondoa Mkude Stars ni sababu za kifamilia.
Wiki chache zilizopita, Jonas Mkude alimpoteza mtoto wake hivyo inaonekana ni miongoni mwa mambo yaliyochangia kuomba aenguliwe.