Fri, 17 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mazungumzo kati ya Menejiment ya Kiungo Fundi Jonas Mkude na klabu ya Yanga yamefikia hatua za mwisho ili mchezaji huyo aweze kusaini kandarasi mpya kuelekea msimu ujao.
Jonas Mkude kuendelea kuwatumikia Wananchi ni pendekezo la Kocha Mkuu Miguel Gamondi kwa Uongozi wa klabu ya Yanga, inatajwa baada ya kumalizika msimu huu ndipo atasaini kandarasi mpya ya mwaka mmoja.
Jonas Mkude ambaye alisaini Yanga mwanzoni mwa msimu huu kwa mkataba wa mwaka mmoja, mpaka sasa hajasaini karatasi zozote za kimkataba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live