Mchambuzi wa soka Bongo, Master Tindwa amesema, kwenye mechi ya Robo Fainali ya Kombe la Mapinduzi, Mkude, Mauya na Ngushi ndio walioiangusha timu ikapoteza kwa 3-1.
Amesema, nyota wengine walipambana sana kuipigania nembo ya Yanga.
“Mshery alikuwa nje muda mrefu hajacheza lakini kiwango alichoonesha anaonekana kabisa huyu ana kitu. Nanguka pia alikuwa na game nzuri sana na mwingine ni Shekhani hata alivyoingia aliongeza kitu.
“Wachezaji hawa wamepewa nafasi na wameonesha wanakitu, Yanga itaangalia inawatumiaje. Lakini kuna wachezaji wazoefu kama Ngushi, Mauya na Mkude wameiangusha Yanga kwa kweli.
“Ukiacha magoli mawili aliyofunga mechi ya kwanza, mechi zingine ameonesha kwanini anakaa nje na Mashabiki wamepata majibu kwanini hawa wanakaa nje,” amesema Master Tindwa.