Wed, 3 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi na Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu wanashuka dimbani kwa Mkapa majira ya saa 1:00 usiku kusaka alama tatu mbele ya Namungo.
Simba ambayo wameanza Ligi kwa kusua sua msimu huu wamecheza michezo minne na kushinda miwili tu.
Katika mchezo huo wa leo jina la kiungo Jonas Mkude limeonekana katika wachezaji watakaoanza mechi ya leo.
Halikadhalika beki Kennedy Juma pia amepata nafasi ya kuanza akichukua nafasi ya beki Henock Inonga mwenye adhabu ya kadi nyekundu.
Jina la beki aliekuwa akifikirisha watu pia, Paschal Wawa lipo kwa wachezaji wa akiba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live