Tue, 1 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Simba SC, Roberto Oliviera amesema anainjoi kuona wachezaji wake wanashambulia kwani ndiyo falsafa yake na falsafa ya Simba.
Robertinho amesema, hapendi kupaki basi halafu atambe kuwa muhimu pointi tatu, anapenda wachezaji wake wacheze kwenye eneo la mwisho la mpinzani wao ili waweze kupata matokeo.
"Narudia hata wapinzani wangu wakisikia hakuna shida, mimi napenda soka la kushambulia," alisema Robertinho akiwa kambini nchini Uturuki.
Simba wanatarajia kurejea nchini kesho alfajiri kwa ajili ya kuuanza msimu mpya wa 2023-24 wa Ligi Kuu ya NBC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live