Wed, 26 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
AL Hilal ya Saudi Arabia ipo hatua za mwisho kukamilisha uhamisho wa straika wa Fulham, Aleksandar Mitrovic, 28.
Taarifa za awali zinaeleza wababe hao wameshafanya makubaliano binafsi na Mitrovic na kinachoendelea ni mazungumzo baina mabosi wa timu zote juu ya ada ya uhamisho.
Awali Fulham iliweka wazi kwamba haina mpango wa kumpiga bei fundi huyu lakini mchezaji amewaambia hataki tena kubaki kwenye timu hiyo
Chanzo: www.tanzaniaweb.live