Sat, 26 Mar 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ni patshika ya kufa mtu katika michezo ya mtoano ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia Qatar 2022.
Katika Uwanja wa Kimataifa Cairo Jijini Cairo,walikutana wana Fainali wawili wa AFCON 2021, Misri dhidi ya Senegal.
Wenyeji Misri wameibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Senegal, bao la kujifunga la beki wa Nancy ya Ufaransa, Saliou Ciss dakika ya nne.
Ushindi huo unawapa matumaini Misri ya kwenda kutafuta suluhu ugenini wiki ijayo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live