Wed, 12 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kama mambo yatakwenda yalivyopangwa kuna uwezekano mkubwa kocha Fred Felix ‘Minziro’ akatua Tanzania Prisons.
Taarifa za uhakika zinasema kuna mazungumzo yanayoendelea ya mkataba baina yake na viongozi wa timu hiyo, ambayo yanafanyika mkoani Dodoma.
Msimu uliopita Minziro alikuwa Geita Gold ambayo ilimaliza katika nafasi ya sita, lakini ikampa mkono wa kwaheri, wakati Prisons ilikuwa na Abdallah Mohamed ‘Bares’ anayetajwa kusaini Mashujaa ya Kigoma iliyopanda Ligi Kuu msimu ulioisha.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live