Thu, 30 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya APR ya Rwanda inakaribia kukamilisha usajili wa Milton Karisa (28) raia wa Uganda ambaye anamaliza mkataba wake na Vipers Sc mwishoni mwa msimu huu.
Mchezaji huyo Karisa atasafiri kuelekea Kigali hivi karibuni kukamilisha uhamisho huo ambapo atasaini mkataba wa miaka mitatu.
APR itaiwakilisha Rwanda katika michuano ya ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao baada ya kuibuka mabingwa nchini kwao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live