Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Milner kusaini Mkataba Mpya Liverpool

Milner Jamessssss.jpeg Kiungo wa Liver, James Milner

Wed, 16 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Liverpool inajiandaa kumpa mkataba mpya mchezaji wake James Milner wa mwaka mmoja zaidi baada ya kocha wa timu hiyo Jurgen Klopp kumuingiza kwenye mipango yake ya msimu ujao.

Mchezaji huyo mwenye miaka 36 mkataba wake wa sasa na klabu ya Liverpool, ambao alisaini mwaka 2019 unafika tamati mwisho wa msimu majira ya kiangazi.

Milner sio tu mchezaji anayeaminiwa zaidi na Klopp, bali ni moja ya kiongozi kwa upande wa mjerumani huyo kwenye vyumba vya kubalishia nguo, na Klopp bado anamuhitaji kuwa sehemu ya timu yake kwa msimu ujao.

Mazungumzo kati ya Milner na Liverpool yanaendelaea na bado hakuna uhakika ni kwa muda gani, mazungungumzo ya kumshawishi kubaki klabuni hapo yatadumu, ikiwa Milner atakubali kubaki kwa msimu ujao ataweka historia ya kucheza kwa misimu 21 mfululizo kwenye ligi kuu ya Uingereza.

Milner ashawai kuzitumikia klabu za Leeds United, Newcastle, Aston Villa, Manchester City na sasa Liverpool pia amefanikiwa kuchukua ubingwa Uingereza, Champions League, UEFA Super Cup na FIFA Club World Cup.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live