Tue, 7 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Yanga imelipa kiasi cha Tsh 50 Million kupitia account ya Rais wa klabu ya Singida Fountain Gate, Japhet Makau kumsajili kiungo mkabaji Yusuph Kagoma ambaye alikuwa kabakiza mkataba wa mwaka mmoja katika klabu hiyo.
Kagoma atajiunga na Young Africans Sports Club kwenye dirisha kubwa kuchukua nafasi ya kiungo Zawadi Mauya.
Kagoma anatarajia kusaini kandarasi ya miaka (2) na Yanga wenye kipengele cha kuongeza miaka (2) mingine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live