Mon, 11 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa zamani wa Liverpool na timu ya Taifa ya England ,Michael Owen amesema siku hizi haoni tena vipaji kwenye mpira ,wachezaji wanaosifiwa kama wachezaji bora ni wenye mbio na nguvu na ili uweze kucheza ni lazima uwe na mbio.
“Hakuna tena vipaji halisi kama zamani,siku hizi ili uwe mchezaji unapimwa kwa kasi , ukiweza kukimbia na ukiwa mwepesi basi unaonekana ni mchezaji mzuri”
“Zamani ilikuwa lazima uwe na skills ili Dunia ikuone mchezaji mzuri”
Je Unakubaliana na Michael Owen?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live