Wed, 17 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jose Mourinho aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa AS Roma mnamo Mei 2021 na kuiongoza klabu hiyo kushinda mechi 60, sare 28 na vipigo 34 kwenye mechi 122.
Aliiongoza AS Roma kutwaa ubingwa wa UEFA Conference League mnamo Mei 25, 2022 pamoja na kuifikisha klabu hiyo kwenye fainali ya UEFA Europa League kabla ya kuondoshwa na Sevila msimu uliopita.
José Mourinho ndani ya AS Roma kama kocha:
Mechi 122
Ushindi ×60
Sare ×28
Vipigo ×34
UEFA Conference League
Leo Januari 16, 2024 baada ya kudumu klabuni hapo kwa zaidi ya miaka miwili Mourinho ameoneshwa mlango wa kutokea.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live