Wed, 31 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliekuwa Straika wa Simba SC Yusuph Mhilu, amefunguka kwa mara ya kwanza tangu kuondoka ndani ya Simba SC.
Mhilu aliesajiliwa na Simba katika Dirisha kubwa la msimu wa 2020/21 amepelekwa Kagera Sugar kwa Mkopo baada ya kukosa nafasi ndani ya kikosi cha Simba.
“Simba ukipewa mechi moja ukacheza chini ya kiwango basi Utakomaa na benchi Hakuna wa kukuuliza una changamoto gani. Kuna wakati mchezaji anatamani mtu sahihi wa Kumuongoza pindi moyo unapopitia Magumu lakini anashindwa.”
Kwa sasa Mhilu yupo katika klabu ya Kagera Sugar alikopelekwa kwa mkopo akitokea Simba SC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live